welcome

dear viewers... karibuni katika blog yetu. kwa mawasiliano zaidi utatupata kwa email nicarwag@gmail.com. simu 0758921901

Monday, July 29, 2013

Nando atolewa ndani ya jumba la Big Brother baada ya kuonesha utovu wa nidham



Breaking News: Nando Disqualified-Elikem gets a Strike
Mshiriki wa kiume toka Tanzania aliyekua anatuwakilisha katika shindano la Big Brother Africa "The Chase" leo ametolewa nje ya jumba hilo na kusitisha uwepo wake katika shindano hilo lililojipatia umaarufu sana barani Afrika.

Tukio hilo limetokea baada ymalumbano kati ya NANDO na ELIKEM yaliyotokea Ijumaa ambapo walitukanana sana, lakini chanzo cha ugomvi huo kikionekana kua ni Nando.


Mbali na ugomvi huo NANDO aliwahi kukamatwa na KISU katika party ya Channel O jumamosi moja akapewa onyo. Ugomvi wa Ijumaa lilikuwa kosa la 2 na kosa la 3 aliloambiwa kwenye diary room ni kuongea maneno ya vitisho dhidi ya ELIKEM kua..."I feel like stabbing him. A nigga like that deserves to die".Pamoja na kukamatwa na Mkasi chini ya kitanda chake, basi bwana NANDO safari yake ikawa imeishia hapo.

NEW SITE IN TOWN

  
Meetnawe is a new social utility that brings all new people together to meet with you. Meetnawe also connects you with your favorite radio programs or tv programs.
     Meetnawe is the combination of two words “Meet” and “Nawe”. Nawe is the Bantu language (Swahili) which is the abbreviation of “Na wewe” which means “With you”. Meetnawe means MEET WITH YOU.

     Electronic media, Meetnawe gives the opportunity to the electronic media (tvs and radios) to create a special account for their programs. By doing so, Meetnawe makes a connection between them and their audiences.

     We thank you for considering us, and we guarantee you that you will enjoy staying with us.

Tuesday, June 18, 2013

Moto wateketeza mali Kariakoo


Hali ikiwa tete.

Moto ukiunguza paa la baa hiyo.

Shock  ya umeme ikitokea karibu na jengo hilo.

Watu waliojaa kushuhudia tukio hilo.

Moto mkubwa umezuka jijini Dar es Salaam karibu kabisa na Soko Kuu la Kariakoo leo asubuhi na kuteketeza baa moja. Chanzo cha moto huo inadaiwa kuwa ni hitilafu ya umeme iliyotokea jirani na baa hiyo.

source: wajanjawatowns.blogspot.com

KONYAGI YAWAPIGA MSASA WABUNGE KUHUSU BIASHARA VIROBA




 Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda cha Konyagi cha Tanzania Distilleries Limited (TDL), David Mgwassa, akionesha kinywaji cha Afrika Kusini kilichofungwa kwenye viroba kama ambavyo Konyagi inafanya hapa nchini.Vinywaji kama hivyo vipo karibu nchi nyingi Ulimwenguni.

 Meneja wa Masoko wa Konyagi, Joseph Chibehe akielezea jinsi vinywaji vyao vinavyochangia mapato ta serikali
 Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kilimo,Maji na Mifugo, Said Nkumba akichangia mada hiyo kwa kuviasa baadhi ya vyombo vya habari kuacha kuandika habari za kudidimiza viwanda vya haba nchini. Kulia ni Idd Azzan Mbunge wa Kinondoni na Dunstan Kitandula ambaye ni Makamu Mwenyekiti was  Kamati ya Bunge ya Uchumi, Viwanda na Biashara.
                               Bidhaa mbalimbali zikiwa zimfungwa kwenye viroba
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda cha Konyagi cha Tanzania Distilleries Limited (TDL), David Mgwassa () akifafanua jambo katika semina ya wajumbe wa Kamati mbili za Bunge za Uchumi,Viwanda na Biashara  pamoja na Kilimo,Maji na Mifugo kuhusu baadhi ya vyombo vya habari vyenye uhusiano na nchi jirani vinavyotumika kupiga vita viwanda vya ndani kikiwemo cha Konyagi. Semina hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki mjini Dodoma.
 Naibu Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo, Amos Makala, akichangia mada katika semina hiyo. Kushoto ni Naibu Waziri wa TAMISEMI, Kassim Majaliwa na Said Nkumba.
 Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Uchumi, Viwanda na Biashara, Dunstan Kitandula akichangia mada hiyo.

Monday, May 27, 2013

FEDHA KESSY NA NANDO WAIWAKILISHA TANZANIA KWENYE SHINDANO LA BIG BROTHER THE CHASE 2013.


IMG_0156
Kundi la Mafikizolo la nchini Afrika Kusini likitoa burudani wakati wa uzinduzi wa show ya Big Brother-The Chase iliyorushwa Live na Channel za DStv 197 na 198 jijini Johannesburg usiku huu. Shindano la Big Brother-The Chase limedhaminiwa na Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel. (Picha na Dewji Blog)
IMG_0140
Baadhi ya wageni waalikwa wakiwemo waandishi wa habari kutoka nchin mbalimbali za Afrika kushuhudia Live uzinduzi huo.
IMG_0209
Mwakilishi kutoka Tanzania Nando akihojiwa na Mtangazaji wa kipindi hicho Ik wakati wa uzinduzi wa show hiyo.Kushoto patna wa Nando Mshiriki kutoka Namibia Cleo.
IMG_0226
Mwakilishi wa Tanzania Fedha Kessy akiwasalimu mashabiki wake kwa kuwapungia bendera ya Tanzania. Kulia ni mtangazaji wa Shindano la Big Brother The Chase 2013 Ik.
IMG_0231
Mtangazaji IK akifanya mahojiano na Patna wa Mwakilishi wa Tanzania Mshiriki kutoka Ghana Elikem wakati wa uzinduzi wa Shindano la Big Brother The Chase lililozinduliwa rasmi leo jijini Johannesburg Afrika Kusini ambapo washiriki watakaa ndani ya jumba hilo kwa siku 90 na mshindi kujinyakulia kitita cha Usd 300,000. Kulia ni Fedha Kessy mshiriki kutoka Tanzania.
IMG_0235
Mtangazaji IK akimtambulisha rasmi mshiriki kutoka Tanzania Fedha Kessy kwa Patna wake Mshiriki kutoka Ghana Elikem wakati wa uzinduzi wa shindano hilo leo jijini Johannesburg.