welcome

dear viewers... karibuni katika blog yetu. kwa mawasiliano zaidi utatupata kwa email nicarwag@gmail.com. simu 0758921901

Tuesday, June 18, 2013

Moto wateketeza mali Kariakoo


Hali ikiwa tete.

Moto ukiunguza paa la baa hiyo.

Shock  ya umeme ikitokea karibu na jengo hilo.

Watu waliojaa kushuhudia tukio hilo.

Moto mkubwa umezuka jijini Dar es Salaam karibu kabisa na Soko Kuu la Kariakoo leo asubuhi na kuteketeza baa moja. Chanzo cha moto huo inadaiwa kuwa ni hitilafu ya umeme iliyotokea jirani na baa hiyo.

source: wajanjawatowns.blogspot.com

KONYAGI YAWAPIGA MSASA WABUNGE KUHUSU BIASHARA VIROBA




 Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda cha Konyagi cha Tanzania Distilleries Limited (TDL), David Mgwassa, akionesha kinywaji cha Afrika Kusini kilichofungwa kwenye viroba kama ambavyo Konyagi inafanya hapa nchini.Vinywaji kama hivyo vipo karibu nchi nyingi Ulimwenguni.

 Meneja wa Masoko wa Konyagi, Joseph Chibehe akielezea jinsi vinywaji vyao vinavyochangia mapato ta serikali
 Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kilimo,Maji na Mifugo, Said Nkumba akichangia mada hiyo kwa kuviasa baadhi ya vyombo vya habari kuacha kuandika habari za kudidimiza viwanda vya haba nchini. Kulia ni Idd Azzan Mbunge wa Kinondoni na Dunstan Kitandula ambaye ni Makamu Mwenyekiti was  Kamati ya Bunge ya Uchumi, Viwanda na Biashara.
                               Bidhaa mbalimbali zikiwa zimfungwa kwenye viroba
 Mkurugenzi Mtendaji wa Kiwanda cha Konyagi cha Tanzania Distilleries Limited (TDL), David Mgwassa () akifafanua jambo katika semina ya wajumbe wa Kamati mbili za Bunge za Uchumi,Viwanda na Biashara  pamoja na Kilimo,Maji na Mifugo kuhusu baadhi ya vyombo vya habari vyenye uhusiano na nchi jirani vinavyotumika kupiga vita viwanda vya ndani kikiwemo cha Konyagi. Semina hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki mjini Dodoma.
 Naibu Waziri wa Habari, Vijana Utamaduni na Michezo, Amos Makala, akichangia mada katika semina hiyo. Kushoto ni Naibu Waziri wa TAMISEMI, Kassim Majaliwa na Said Nkumba.
 Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Uchumi, Viwanda na Biashara, Dunstan Kitandula akichangia mada hiyo.